SERIKALI KUTOA NAKALA ZA RIPOTI KWA MAANDISHI YA NUKTA NUNDU ILI KUWASAIDIA WATU WENYE ULEMAVU WA KUTOONA.





TAREHE 22-09-2017
CAG  PROFESSA  MUSSA ASSAD

Mkaguzi na mdhibiti mkuu wa hesabu za serikali CAG Professa Mussa Assad amesema kuwa ofisi yake iko kwenye mchakato wa kutoa nakala za ripoti zake kwa maandishi ya nukta nundu ili kuwasaidia  watu wenye ulemavu wa kutoona.

Professa Assad ameyasema hayo wakati akifungua warsha kuhusu namna ya kusambaza na kukusanya maoni ya toleo maalumu kwa mwaka wa fedha wa 2015-2016 mjini Moshi,ambapo amesema kuwa ripoti hizo zitaanza kutolewa kwa maandishi katika mwaka ujao wa fedha.


Amesema kuwa kituo cha usambazaji na ukusanyaji wa maoni ya toleo maalumu za mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali ni cha nne na kimeshirikisha asasi za kiraia kutoka mikoa ya Arusha,Kilimanjaro,Manyara na Tanga.
SERIKALI KUTOA NAKALA ZA RIPOTI KWA MAANDISHI YA NUKTA NUNDU ILI KUWASAIDIA WATU WENYE ULEMAVU WA KUTOONA. SERIKALI   KUTOA  NAKALA  ZA   RIPOTI  KWA  MAANDISHI  YA  NUKTA  NUNDU   ILI  KUWASAIDIA   WATU    WENYE   ULEMAVU    WA   KUTOONA. Reviewed by safina radio on September 22, 2017 Rating: 5

No comments