NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI MH. MERNAD KALEMANI AMELIAGIZA JESHI LA POLISI MKOANI SINGIDA KUMKAMATA MENEJA WA SHIRIKA LA UMEME TANZANIA TANESCO WA MJI WA ITIGI .
14-09-2017
![]() |
NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI KUSHOTO MH. MERNAD KALEMANI. |
Naibu waziri
wa nishati na madini Mh Mernad Kalemani ameliagiza jeshi la polisi mkoani
Singida kumtafuta na kumkamata meneja wa shirika la umeme Tanzania Tanesco wa
mji wa Itigi anayetuhumiwa kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu kutoka kwa
wananchi wa mji huo.
Mh Kalemani
ametoa maagizo hayo wakati akihutubia katika mkutano wa hadhara uliofanyika
katika mji wa Itigi mkoani Singida,ambapo amesema kuwa meneja huyo ambaye ni Bw
Ramadhan Rajabu alijipatia kiasi cha shilingi milioni 60 baada ya kuwarubuni
wananchi kwamba atawaunganishia umeme na kuwapa risiti bandia.
Aidha
kutokana na udanganyifu huo naibu waziri huyo amelitaka shirika la umeme
kuwaunganishia huduma ya umeme wananchi mia tano wa mji huo waliokatiwa umeme
baada ya kukutwa na risiti bandia na ambao wamejiunganishia huduma ya umeme
kinyemela baada ya kubainika kuwa hawana hatia.
Hata hivyo
Dr Kalemani alikuwa mkoani Singida katika mji wa Itigi kwa lengo la kusikiliza
na kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi. Naibu waziri
wa nishati na madini Mh Mernad Kalemani ameliagiza jeshi la polisi mkoani
Singida kumtafuta na kumkamata meneja wa shirika la umeme Tanzania Tanesco wa
mji wa Itigi anayetuhumiwa kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu kutoka kwa
wananchi wa mji huo.
NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI MH. MERNAD KALEMANI AMELIAGIZA JESHI LA POLISI MKOANI SINGIDA KUMKAMATA MENEJA WA SHIRIKA LA UMEME TANZANIA TANESCO WA MJI WA ITIGI .
Reviewed by safina radio
on
September 14, 2017
Rating:

No comments