MBUNGE WA VITI MAALUM MKOA WA ARUSHA MH. AMINA MOLLEL AIOMBA SERIKALI KUIPATIA MAJI SHULE YA SEKONDARI MLANGARINI
TAREHE 18-09-2017
![]() |
MBUNGE WA VITI MAALUM MKOA WA ARUSHA MH. AMINA MOLLEL |
Mbunge wa viti maalum mkoa wa Arusha Mh Amina Mollel ameiomba
serikali kuipatia maji shule ya sekondari Mlangarini kwani kwa sasa
inakabiliwa na changamoto hiyo hali ambayo inaweza kuleta madhara kwa
wanafunzi.
Mh Amina Mollel ametoa maombi hayo mbele ya mkuu wa mkoa wa Arusha
Bw Mrisho Gambo mara baada ya kufanya ziara shuleni hapo kwa lengo la kubaini
changamoto zinazoikabili shule hiyo.
Amefafanua kuwa kutokana na tatizo hilo wanafunzi wa shule hiyo hulazimika
kufuata maji mtoni na kuhatarisha maisha ya wanafunzi hao hasa wa kike ambao hunusirika kubakwa hivyo
shule hiyo inatakiwa kupatiwa mradi wa maji haraka iwezekanavyo ili kusogeza
huduma karibu na wanafunzi.
Akijibu kero hiyo kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Arusha mkurugenzi
wa halmashuri ya wilaya ya Arusha Dk Wilson Mahera amesema kuwa changamoto
hiyo itatatuliwa mapema iwezekanavyo kwani tayari upo mradi wa benki ya dunia
unaopita maeneo hayo hivyo wanafunzi hao hawatakiwi kuwa na wasiwasi.
MBUNGE WA VITI MAALUM MKOA WA ARUSHA MH. AMINA MOLLEL AIOMBA SERIKALI KUIPATIA MAJI SHULE YA SEKONDARI MLANGARINI
Reviewed by safina radio
on
September 18, 2017
Rating:

No comments