WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MH. MAJALIWA KASSIMU MAJALIWA AMESEMA SERIKALI ITAENDELEA KUPELEKA FEDHA KWENYE MIRADI MBALIMBALI YA MAENDELEO.

TAREHE 15-09-2017



WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MH. MAJALIWA KASSIMU MAJALIWA

Waziri mkuu wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mh Majaliwa Kassimu Majaliwa  amesema kuwa serikali itaendelea kupelekeka fedha kwenye miradi mbalimbali ya maendeleo hapa nchini ikiwemo sekta ya afya.

Mh Majaliwa ameyasema hayo leo bungeni mjini Dodoma wakati akitoa hotuba ya kuharisha mkutano wa nane wa bunge ulioanza Septemba 05 mwaka huu,ambapo amesema kuwa nia ya serikali kupeleka fedha hizo ni ili kutatua changamoto  zinazowakabili wananchi wa maeneo mbalimbali hapa nchini.

Amesema kuwa katika sekta ya afya kwa mwaka wa fedha wa 2017/2018 upatikanaji wa dawa katika bohari ya dawa nchini MSD umeongezeka hadi kufikia asilimia 82 ikilinganishwa na wastani wa asilimia 50 kwa kipindi cha mwaka 2016/2017,ambapo pia upatikanaji wa dawa umeongezeka katika vituo vya afya hadi kufikia asilimia 90 ikilinganishwa na asilimia 60 za hapo awali.


Amesema kuwa mafanikio hayo yanatokana na juhudi za serikali kuongeza bajeti katika sekta ya afya nchini kutoka kiasi cha shilingi trilioni 1.988 mwaka wa 2016/2017 hadi kufikia trilioni 2.222 kwa mwaka wa fedha wa 2017/2018 ambapo ongezeko hilo ni sawa na asilimia 11.77.
WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MH. MAJALIWA KASSIMU MAJALIWA AMESEMA SERIKALI ITAENDELEA KUPELEKA FEDHA KWENYE MIRADI MBALIMBALI YA MAENDELEO. WAZIRI   MKUU  WA  JAMHURI  YA  MUUNGANO  WA  TANZANIA  MH.  MAJALIWA  KASSIMU MAJALIWA  AMESEMA  SERIKALI  ITAENDELEA   KUPELEKA   FEDHA   KWENYE  MIRADI  MBALIMBALI  YA  MAENDELEO. Reviewed by safina radio on September 15, 2017 Rating: 5

No comments