WATU SABINI WAMEUAWA NA WENGINE KUJERUHIWA BAADA YA MASHAMBULIZI MAWILI YA KUJITOA MUHANGA NCHINI IRAQ .





TAREHE 15-09-2017


PICHA YA SHAMBULIZI LA KIGAIDI



Kundi linalojiita Dola la Kiislamu , limedai kuhusika na mashambulizi mawili ya kujitoa muhanga nchini Iraq ambapo watu 70 wameuwawa na wengine wengi wamejeruhiwa.

Maafisa nchini humo wamesema idadi ya watu waliouwawa huenda ikapanda kutokana na watu wengi waliojeruhiwa kuwa katika hali mbaya .

Washambuliaji walishambulia hoteli pamoja na kituo cha polisi cha upekuzi karibu na mji wa kusini mwa Iraq wa Nasiriyah siku ya Alhamis,ambapo Mahujaji kadhaa wa Iran ni miongoni mwa waliouwawa.


Hata hivyo eneo lililoshambuliwa liko katika barabara kuu inayotumiwa na mahujaji wa Kishia na watu wanaotembelea eneo hilo kutoka magharibi mwa Iran kusafiri kwenda katika miji mitakatifu ya Najaf na Karbala upande wa kaskazini.
WATU SABINI WAMEUAWA NA WENGINE KUJERUHIWA BAADA YA MASHAMBULIZI MAWILI YA KUJITOA MUHANGA NCHINI IRAQ . WATU  SABINI WAMEUAWA  NA  WENGINE  KUJERUHIWA  BAADA  YA  MASHAMBULIZI  MAWILI  YA  KUJITOA  MUHANGA NCHINI  IRAQ . Reviewed by safina radio on September 15, 2017 Rating: 5

No comments