WATU WATATU AKIWEMO AFISA WA POLISI WAUAWA KATIKA SHAMBULIZI LA KIGAIDI HUKO AFGHANISTAN



TAREHE 14-09-2017
WANAJESHI WAKIWA KATIKA MJI MKUU WA AFGHANISTAN KABUL



Mshambuliaji wa kujitoa muhanga amejilipua karibu na uwanja wa mchezo wa kriketi katika mji mkuu wa Afghanistan, Kabul na kuua watu watatu akiwemo afisa wa polisi.

 Duru za polisi zinasema watu wengine watano walijeruhiwa katika shambulizi hilo wakiwemo maafisa wawili wa polisi.

Mshambuliaji huyo alijilipua baada ya kusimamishwa katika kituo cha upekuzi na maafisa wa polisi waliomshuku wakati alipokuwa akitembea kuelekea uwanja huo ambako mechi ilikuwa ikiendelea.


Hata hivyo kitengo cha Kundi la dola la kiislamu katika mkoa wa Khorasan kimedai kuhusika na hujuma hiyo.
WATU WATATU AKIWEMO AFISA WA POLISI WAUAWA KATIKA SHAMBULIZI LA KIGAIDI HUKO AFGHANISTAN WATU WATATU AKIWEMO AFISA WA POLISI WAUAWA KATIKA SHAMBULIZI LA KIGAIDI  HUKO AFGHANISTAN Reviewed by safina radio on September 14, 2017 Rating: 5

No comments