WAFUGAJI WILAYANI BABATI MKOANI MANYARA WAHIMIZWA KUTUMIA MIFUGO WALIYONAYO KUBORESHA MAISHA YAO.
TAREHE 27-09-2017
Wafugaji wa Halmashauri ya Wilaya ya
Babati mkoani Manyara wamehimizwa kutumia raslimali ya mifugo waliyonayo
kuboresha maisha ya familia, kuwekeza katika elimu kwa kuwapeleka watoto
wao shule na kuchangia mipango ya maendeleo katika maeneo yao.
Ushauri huo umetolewa na Mkuu wa
Wilaya ya Babati Mkoani humo Bw Raymond Mushi wakati akizindua zoezi la upigaji
chapa ng’ombe katika kijiji cha Ngoley kata ya Mwada,ambapo amesema kuwa idadi ya mifugo inayofugwa ni lazima
ilingane na eneo la malisho ili ufugaji uwe wenye tija.
Amesema wafugaji wakitumia rasilimali
walizonazo ambazo ni mifugo kwa tija wataweza kufuga kisasa na kuboresha maisha
yao ambayo yatasaidia kuinua kipato cha mtu mmoja mmoja na taifa ikiwa ni
pamoja na kuinua uchumi wa mkoa huo.
Aidha amesema zoezi hilo la kupiga
chapa Ngombe
hao ni agizo la Serikali kupitia wizara ya
Kilimo,Mifugo na Uvuvi la kuanza upya zoezi la kuweka alama ng’ombe ili
kutimiza sheria ya utambuzi usajili na ufuatiliaji mifugo kifungu cha 5(1) cha
sheria namba 12 ya mwaka 2010 inayoelekeza mifugo yote kufanyiwa
Utambuzi,Usajili na Ufuatiliaji.
Bw Mushi ametaja faida za zoezi la Utambuzi,Usajili na
Ufuatiliaji mifugo kuwa ni kudhibiti magonjwa ya mifugo,wizi wa
mifugo,kupunguza migogoro kati ya wakulima na wafugaji, kuhakikisha usalama wa
chakula cha mifugo na kuboresha bidhaa zitokanazo na mifugo.
Kwa upande wake Mkurugenzi mtendaji wa
Halmashauri ya Wilaya ya Babati Bw Hamisi Malinga amesema kuwa tangu zoezi hilo
kuanza Julai 2017 kwa kutoa elimu, uhamasishaji na uandaaji wa vifaa jumla ya Ng’ombe
elfu nne mia saba na sabini wamepigwa
chapa.
WAFUGAJI WILAYANI BABATI MKOANI MANYARA WAHIMIZWA KUTUMIA MIFUGO WALIYONAYO KUBORESHA MAISHA YAO.
Reviewed by safina radio
on
September 27, 2017
Rating:

No comments