RAIS WA MAREKANI DONALD TRUMP ASAINI SHERIA MPYA YA KUONGEZA VIKWAZO DHIDI YA KOREA YA KASKAZINI



TAREHE 22-09-2017
RAIS WA  MAREKANI  DONALD TRUMP

Rais wa Marekani Donald Trump amesaini sheria mpya ya kuongeza vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini juu ya mpango wake wa nyuklia.

Waziri wa fedha wa Marekani ameidhinisha vikwazo hivyo dhidi ya makampuni ya fedha yanayofanya biashara zake ndani ya Korea Kaskazini.

Rais Trump pia amesema kuwa Benki Kuu ya Uchina iliagiza benki nyingine za Uchina kuacha kufanya biashara na Korea Kaskazini.

Hatua hii inakuja katika kipindi cha chini ya wiki mbili baada ya Umoja wa Mataifa kuidhinisha vikwazo vipya dhidi ya taifa hilo kwasababu ya jaribilo lake la hivi karibuni la nyuklia.


Hali ya wasiwasi imetanda katika kipindi cha wiki za hivi karibuni kutokana na hatua ya Korea Kaskazini kufanya majaribio ya makombora ya masafa marefu, licha ya shinikizo kutoka kwa mataifa tajiri zaidi duniani.
RAIS WA MAREKANI DONALD TRUMP ASAINI SHERIA MPYA YA KUONGEZA VIKWAZO DHIDI YA KOREA YA KASKAZINI RAIS  WA  MAREKANI  DONALD  TRUMP  ASAINI   SHERIA   MPYA   YA   KUONGEZA VIKWAZO  DHIDI  YA  KOREA  YA  KASKAZINI Reviewed by safina radio on September 22, 2017 Rating: 5

No comments