KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MIUNDOMBINU YAISHAURI SERIKALI KUWEKA ALAMA YA UTAMBUZI KATIKA MIRADI YAKE
tarehe 22-09-2017
![]() |
Kamati ya
kudumu ya bunge ya miundombinu imeishauri serikali kuweka alama ya utambuzi kwenye
miradi yake yote wanayoijenga ili wananchi waweze kufahamu kazi inayofanywa na
serikali yao.
Kamati hiyo
imetoa kauli hiyo wakati baada ya kutembelea miundombinu ya mawasiliano katika wilaya ya
Mkuranga mkoani Pwani ili kuona maendeleo yake lengo likiwa ni kuhakikisha miradi
hiyo ikiwemo ya mawasiliano inakamiliaka kwa wakati ili wananchi waweze kupata
mawasiliano.
Akizungumza
wakati mara baada ya kutembelea miradi hiyo,makamu mwenyekiti wa wa kamati hiyo
Mh Juma Kakoso,amesema kuwa pale serikali itakapoweka alama za utambuzi katika
miradi yake itasaidia wananchi kuona kazi kubwa inayofanywa na serikali yao
katika kuwaletea maendeleo ikiwemo miundombinu ya minara ya mawasiliano ya
simu.
Kwa upande
wake katibu wa mfuko wa mawasiliano kwa wote Justina Mashiba amesema kuwa zaidi
minara mia nne hapa nchini inafanya kazi ili kusaidia upatikanaji wa
mawasiliano kwa wananchi na uwekaji wa alama za utambuzi umekwishaanza.
KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MIUNDOMBINU YAISHAURI SERIKALI KUWEKA ALAMA YA UTAMBUZI KATIKA MIRADI YAKE
Reviewed by safina radio
on
September 22, 2017
Rating:

No comments