SERIKALI KUTAFUTA WAWEKEZAJI KUJA KUWEKEZA KWENYE ZAO LA TANGAWIZI


TAREHE 14 -09-2017

ZAO LA TANGAWIZI


Ili kuhakikisha kuwa zao la tangawizi linapata soko hapa nchini na nje ya nchi serikali imesema kuwa  inaendelea kuhamasisha na kushawishi sekta binafsi kuja kuwekeza katika zao la viungo ikiwemo tangawizi pamoja na kutafuta wateja wa zao hilo kupitia maonesho mbalimbali ya kibiashara.

Hayo yamesemwa leo bungeni mjini Dodoma na waziri wa viwanda,biashara na uwekezaji Mh Charles Mwiijage wakati akijibu swali la mbunge wa kuteuliwa Mh Anna Kilango Malechela aliyetaka kujua serikali ina mpango gani wa kutafuta soko la tangawizi ili wananchi wanaolima zao hilo wapate sehemu kuuzia.

Mh Mwiijage ameongeza kuwa ili kuhakikisha bidhaa ya tangawizi inayouzwa katika soko la ndani la nje inakidhi ubora unaotakiwa serikali imejenga maabara ya chakula yenye hadhi ya kimataifa ili kuwawezesha wazalishaji wa zao hilo kufikia viwango vinavyotakiwa na masoko ya nje.


Ameongeza kuwa mpaka sasa kuna makampuni 21 ambayo yanajishughulisha na shughuli za uuzaji viungo nje ya nchi ikiwemo tangawizi,hivyo juhudi za serikali ni kuona kuwa makampuni hayo yanakuwa na uwezo wa kuuza bidhaa hiyo ndani na nje ya nchi ili kuinua uchumi wa taifa na wa mkulima.





SERIKALI KUTAFUTA WAWEKEZAJI KUJA KUWEKEZA KWENYE ZAO LA TANGAWIZI SERIKALI KUTAFUTA  WAWEKEZAJI KUJA KUWEKEZA KWENYE ZAO LA TANGAWIZI Reviewed by safina radio on September 14, 2017 Rating: 5

No comments