WANAWAKE NCHINI SAUDIA ARABIA KUPEWA LESENI ZA KUENDESHA MAGARI.

TAREHE 27-09-2017  



Vyombo vya habari vya serikali ya Saudi Arabia vimeripoti kuwa kuanzia Juni mwakani wanawake nchini humo watapewa leseni za kuendesha magari ambazo zitawawezesha kuendesha magari kwa mara ya kwanza katika taifa hilo la kifalme.

Chombo maalumu cha kiserikali kinatarajiwa kuundwa ndani ya siku 30 ili kutekeleza amri hiyo ifikapo Juni 2018.

 Wakati huohuo balozi wa Saudi Arabia kwenye Umoja wa Mataifa mwana wa mfalme Khaled bin Salman amewaambia waandishi wa habari kuwa wanawake hawatakuwa na ulazima wa kuwa na mtu ndani ya gari kwa ajili ya kuwasimamia wakati watakapokuwa wanaendesha magari.


 Amesema kuwaruhusu wanawake kuendesha magari ni hatua kubwa nchini humo,ambapo Saudi Arabia ni nchi pekee ulimwenguni ambayo wanawake hawaruhusiwi kuendesha magari.
WANAWAKE NCHINI SAUDIA ARABIA KUPEWA LESENI ZA KUENDESHA MAGARI. WANAWAKE    NCHINI    SAUDIA   ARABIA   KUPEWA   LESENI  ZA   KUENDESHA  MAGARI. Reviewed by safina radio on September 27, 2017 Rating: 5

No comments