WAZIRI WA NCHI OFISI YA RAIS UTUMISHI NA UTAWALA BORA MH. ANGELA KAIRUKI AMESEMA ILI KUHAKIKISHA FEDHA ZA TASAF ZINANUFAISHA WALENGWA SERIKALI IMEONDOA KAYA ZAIDI YA ELFU 76
TAREHE 15-09-2017
![]() |
WAZIRI WA NCHI OFISI YA RAIS NA UTAWALA BORA MH. ANGELA KAIRUKI |
Waziri wa nchi
ofisi ya rais utumishi na utawala bora Mh Angela Kairuki amesema kuwa ili
kuhakikisha fedha zinazotolewa na mfuko wa kuhudumia kaya maskini yaani TASAF
inawanufaisha walengwa,serikali imefanikiwa kuondoa zaidi ya kaya elfu 76
ambazo ziliingizwa kimakosa katika mfuko huo.
Mh Kairuki
ameyaseam hayo leo bungeni mjini Dodoma wakati akijibu swali la mbunge wa viti
maalumu Mh Nuru Fadhili aliyetaka kujua serikali inachukua hatua gani kwa kaya
zinazohudumiwa na mfuko huo wa TASAF na wakati hawastahili kuwepo katika orodha
ya kuhudumiwa kama watu maskini.
Amesema kuwa
moja ya sababu inayosababisha kaya ambazo hazistahili kuingizwa kwenye orodha
ya kuhudumiwa na TASAF ni kutokana na itikadi za kisiasa kutumika katika
mikutano mikuu ya vijiji ambayo ndiyo inayorodhesha kaya hizo.
Kutokana na
taizo hilo Mh Kairuki amewaomba wananchi pamoja na viongozi wa vijiji
kushirikiana na serikali katika kuwabaini wale wote waliorodheshwa kimakosa
katika mfuko huo ili waweze kuondolewa ili kaya zinazostahili ziweze kupata
fedha hizo zitakazosaidia kuwapunguzia hali ya umaskini waliyonayo.
Hata hivyo
tangu mfuko wa kuhudumia kaya maskini TASAF uanzishwe mwaka wa 2000 imefanikiwa
kuwasaidia watu wenye hali ya umaskini kupata huduma za
afya,elimu,maji,barabara na chakula.
WAZIRI WA NCHI OFISI YA RAIS UTUMISHI NA UTAWALA BORA MH. ANGELA KAIRUKI AMESEMA ILI KUHAKIKISHA FEDHA ZA TASAF ZINANUFAISHA WALENGWA SERIKALI IMEONDOA KAYA ZAIDI YA ELFU 76
Reviewed by safina radio
on
September 15, 2017
Rating:

No comments