MKUU WA WILAYA YA LINDI SHAHIDI NDEMANGA AMEITAKA MAMLAKA YA MAPATO TANZANIA TRA KUDHIBITI NA KUCHUKUA HATUA KWA YEYOTE ATAKAYEINGIZA BIDHAA KWA KUPITIA BANDARI BUBU KATIKA WILAYA HIYO.
![]() |
MKUU WA WILAYA YA LINDI BW. SHAHIDI NDEMANGA |
Mkuu wa
wilaya ya Lindi Shaidi Ndemanga ameitaka mamlaka ya mapato Tanzania TRA mkoa wa
Lindi kudhibiti na kuchukua hatua kali mfanyabiashara yeyote atakayeingiza
bidhaa kwa njia ya magendo kupitia bandari bubu zilizoko katika wilaya hiyo.
Bw Ndemanga
ametoa kauli hiyo wakati wa operesheni maalumu ya kuzuia magendo iliyofanyika
katika mwambao mwa bahari ya Hindi ,ambapo amesema kuwa bandari ambazo TRA inatakiwa
kuzuia bidhaa za magendo kuingia ni bandari za Mchinga,Shuka na Sudi.
Amesema kuwa
endapo TRA itazuia magendo hayo serikali itaweza kupata mapato mengi na wale
watakaokamatwa wanajihusisha na biashara hiyo haramu watachukuliw hatua kali za
kisheria ikiwemo kufungwa jela ili iwe fundisho kwa wengine.
Hata hivyo
katika operesheni hiyo imekamatwa shehena mbalimbali za mizigo ikiwemo mifuko
mia moja arobaini na tano ya sukari na madumu ya mafuta ya kupukia 76 yenye
thamani ya shilingi milioni sita.
MKUU WA WILAYA YA LINDI SHAHIDI NDEMANGA AMEITAKA MAMLAKA YA MAPATO TANZANIA TRA KUDHIBITI NA KUCHUKUA HATUA KWA YEYOTE ATAKAYEINGIZA BIDHAA KWA KUPITIA BANDARI BUBU KATIKA WILAYA HIYO.
Reviewed by safina radio
on
September 15, 2017
Rating:

No comments