MKUU WA MKOA WA DAR -ES SALAAM PAUL MAKONDA AMEZIELEKEZA MANISPAA ZOTE ZA MKOA HUO KUTOA MIKOPO NAFUU KWA WAJASIRIAMALI

TAREHE 28-09-2017

MKUU  WA  MKOA   WA  DAR ES  SALAAM   PAUL    MAKONDA
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Bw. Paul Makonda amezielekeza manispaa zote za mkoa huo  kutoa mikopo nafuu kwa wajasiriamali wenye viwanda vidogovidogo  ili kuweza kusaidia katika uanzishwaji wa viwanda  mkoani humo

Bw Makonda ametoa agizo hilo  jijini Dar es salaam  wakati akizungumza na waandishi wa habari namna alivyojipanga kusaidia wananchi wake kiuchumi,ambapo amesema kuwa kuna asilimia kumi za fedha katika kila manspaa za mkoa huo tano kwa ajili ya akina mama na tano kwa ajili ya vijana hivyo watatumia fedha hizo ili waweze kuanzisha viwanda vidogovidogo.

Amesema kuwa amefanya mzungumzo na  mfuko wa hifadhi ya jamii NSSF  ili kuweza kutoa mikopo nafuu na kusaidi wafanya biashara katika kuanzisha viwanda vidogovidogo na kuwa taka wafanya biashara  hao kufika ofisi ya mkoa  kujiandisha ili wapewe mikopo hiyo.


Hata hivyo mkuu huyo wa mkoa  amesema kuwa ataanzisha soko la kuuza bidhaa zilizotengenezwa na viwanda vya ndania jijini Dar es salaam hivyo,amewataka wamachinga kuuza bidhaa zinazozalishwa hapa nchini ili kukuza uchumi wa taifa na kuongeza ajira kwa watanzania haswa vijana.
MKUU WA MKOA WA DAR -ES SALAAM PAUL MAKONDA AMEZIELEKEZA MANISPAA ZOTE ZA MKOA HUO KUTOA MIKOPO NAFUU KWA WAJASIRIAMALI MKUU   WA   MKOA    WA  DAR -ES SALAAM   PAUL  MAKONDA    AMEZIELEKEZA   MANISPAA  ZOTE   ZA   MKOA   HUO  KUTOA   MIKOPO    NAFUU   KWA    WAJASIRIAMALI Reviewed by safina radio on September 28, 2017 Rating: 5

No comments