SERIKALI KUENDELEA KUZIJENGEA UWEZO TAASISI ZA UONGOZI HAPA NCHINI


tarehe 22-09-2017

WAZIRI  WA NCHI  OFISI YA RAIS NA UTAWALA MH. ANGELA KAIRUKI
Waziri wa nchi ofisi ya rais utumishi na utawala bora Mh Angela Kairuki amesema kuwa,serikali itaendelea kuzijengea uwezo taasisi za uongozi nchini ili ziweze kutoa mafunzo kwa viongozi wa kada mbalimbali kwa lengo la kuharakisha maendeleo ya taifa.

Mh Kairuki ameyasema hayo jijini Dar-es-salaam wakati wa uzinduzi wa bodi mpya ya taasisi ya viongozi nchini,ambapo amesema kuwa zaidi ya viongozi elfu moja na mia saba wamepata mafunzo kutoka taasisi ya uongozi, mafunzo ambayo yamewajengea ufanisi katika utendaji wao wa kazi.

Amesema kuwa serikali imeingia mkataba wa miaka minne na serikali ya Finland katika kuboresha utendaji wa taasisi hiyo kwa lengo la kuwandaa viongozi watarajiwa watakaokuwa na weledi katika utendaji wao wa kazi.


Hata hivyo waziri Kairuki amesema serikali ina mango wa kuandaa tovuti maalumu ya kuratibu majina ya viongozi watakaokuwa tayari kushika nyadhifa mbalimbali serikalini pale watakapohitajika.
SERIKALI KUENDELEA KUZIJENGEA UWEZO TAASISI ZA UONGOZI HAPA NCHINI SERIKALI   KUENDELEA   KUZIJENGEA   UWEZO   TAASISI  ZA  UONGOZI   HAPA   NCHINI Reviewed by safina radio on September 22, 2017 Rating: 5

No comments