WATU 8 WAMEFARIKI DUNIA NA WENGINE 12 KUJERUHIWA NCHINI MAREKANI.

TAREHE 1-11-2017

Marekani
Image captionShambulizi Meya wa mji wa New York, Bill De Blasio, amesema kwamba watu 8 wamefariki dunia na zaidi ya 12 wamejeruhiwa baada ya  gari kuwagonga waendesha baiskeli mjini humo.
Kwa upande wake Kamishna wa polisi wa jiji la New York, James O'Neill, amemuelezea mtu aliyetekeleza tukio hilo kuwa ni kijana wa miaka 29 aliyekuwa anaendesha gari ndogo la kubebea mizigo alilokuwa amelikodi.
O`Nell Amesema gari hilo liliwagonga watembea kwa miguu na wapanda baiskeli kabla ya kugongana na basi la shule.
Polisi mjini humo wametoa tamko kwamba wanalichukulia tukio hilo kama shambulizi la kigaidi , Mtuhumiwa wa tukio hilo amechukuliwa na polisi kwa mahojiano zaidi  katika kituo cha Lower Manhattan.

Hata hivyo Vyombo vya habari nchini Marekani vimenukuu taarifa za polisi kuwa kijana huyo aliamua kuendesha gari hilo katika njia ya waendesha baisikeli iliyoko karibu na Mto Hudson eneo la Lower Manhattan ya chini ,kabla ya kupigwa risasi na maafisa wa polisi ili kuzuia shambulio alilolipanga.
WATU 8 WAMEFARIKI DUNIA NA WENGINE 12 KUJERUHIWA NCHINI MAREKANI. WATU  8 WAMEFARIKI DUNIA NA WENGINE 12  KUJERUHIWA NCHINI MAREKANI. Reviewed by safina radio on November 01, 2017 Rating: 5

No comments