MAREKANI YAIONYA KOREA KASKAZINI

TAREHE 30-11-2017


Marekani imeuonya utawala wa Korea Kaskazini kuwa utaangamizwa kabisa iwapo vita vitazuka baada ya Korea Kaskazini hapo jana kurusha kombora la masafa marefu ambalo lilisemekana lina uwezo wa kufika kokote  nchini Marekani.

Akizungumza katika mkutano wa dharura wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, balozi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa, Nikki Haley amesema hawajawahi kutafuta kuingia vitani na Korea Kaskazini, lakini iwapo vitazuka, itakuwa ni kutokana na vitendo vya kichokozi kama walivyoshuhudia jana hali inayoweza kuifanya nchini hiyo kusaharibiwa kabisa.

Naye waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani, Sigmar Gabriel amesema Korea Kaskazini imekiuka sheria za kimataifa na kwamba vitendo hivyo vinatishia usalama wa kimataifa.


Kwa upande wake rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amesema anatumai China na Urusi zitaiongezea Korea Kaskazini vikwazo ili kuishinikiza kuachana na mpango wake wa kinyuklia na kurusha makombora.
MAREKANI YAIONYA KOREA KASKAZINI MAREKANI  YAIONYA KOREA KASKAZINI Reviewed by safina radio on November 30, 2017 Rating: 5

No comments