MAHAKAMA YA ICC YAIDHINISHA UCHUNGUZI DHIDI YA MADAI YA UHALIFU YALIYOFANYWA KWA AMRI SERIKALI YA BURUNDI

TAREHE 10-11-2017

Majaji wa mahakama ya kimataifa ya makosa ya uhalifu, ICC wameidhinisha uchunguzi kuhusu madai ya uhalifu yaliyofanywa kwa amri ya serikali nchini Burundi ambayo ni pamoja na mauaji, ubakaji na utesaji.

Majaji hao wamesema vithibitisho vilivyotolewa na waendesha mashitaka vinatoa sababu ya msingi ya kuendelezwa kwa uchunguzi wa makosa ya uhalifu yaliofanyika tangu Aprili 26 2015, yanayodaiwa kufanywa na mawakala wa serikali na makundi yanayotekeleza sera ya serikali.


 Burundi iliingia katika ghasia na mamia ya raia kupoteza maisha mwaka 2015, baada ya rais Pierre Nkurunziza kutangaza nia yake ya kuwania awamu ya tatu ya urais, ambayoalishinda. Matukio hayo ya uhalifu ayanadaiwa kutendwa na jeshi la polisi la Burundi, usalama wa taifa, vikosi vya jeshi na makundi ya umoja wa vijana wa chama tawala yajulikanayo kama Imbonerakure.
MAHAKAMA YA ICC YAIDHINISHA UCHUNGUZI DHIDI YA MADAI YA UHALIFU YALIYOFANYWA KWA AMRI SERIKALI YA BURUNDI MAHAKAMA  YA  ICC  YAIDHINISHA UCHUNGUZI DHIDI  YA MADAI YA UHALIFU YALIYOFANYWA  KWA  AMRI SERIKALI  YA BURUNDI Reviewed by safina radio on November 10, 2017 Rating: 5

No comments