WANAJESHI NCHINI ZIMBABWE WAMUWEKA MUGABE KWENYE KIZUIZI CHA NYUMBANI.

TAREHE 16-11-2017

Wanajeshi wa Zimbabwe wamemuweka rais Robert Mugabe kwenye kizuizi cha nyumbani katika hatua inayoonekana kuwa wanajeshi hao wametwaa mamlaka ya nchi hiyo.

Hata hivyo meja jenerali Sibusiso Moyo amesema lengo lao ni kuwakabili wahalifu wanaomzunguka rais Mugabe na sio kuipindua serikali. Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma alizungumza na rais Mugabe na kuthibitisha kwamba kiongozi huyo wa Zimbabwe anazuiliwa nyumbani kwake.

Akizungumzia juu ya hali ya nchini Zimbabwe katibu mkuu wa Umoja wa mataifa Antonio Guterres ametoa mwito wa utulivu na subira.


Rais wa Umoja wa Afrika Alpha Conde amelaani hatua ya wanajeshi wa Zimbabwe ya kutwaa mamlaka ya nchi hiyo,ambapo amewataka wanajeshi hao warejee kambini ili kuiheshimu katiba. 
WANAJESHI NCHINI ZIMBABWE WAMUWEKA MUGABE KWENYE KIZUIZI CHA NYUMBANI. WANAJESHI NCHINI ZIMBABWE WAMUWEKA MUGABE KWENYE KIZUIZI CHA NYUMBANI. Reviewed by safina radio on November 16, 2017 Rating: 5

No comments