WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI MHANDISI ISACK KAMWELWE AMESEMA SERIKALI IMEFANIKIWA KUTOKOMEZA MAGONJWA YA MILIPUKO.

TAREHE 29-11-2017


Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Isack Kamwelwe amesema Serikali imefanikiwa kutokomeza magonjwa ya milipuko katika maeneo ya Kilimahewa, Kitangire na Kirumba katika Manispaa ya Ilemela Jijini Mwanza baada ya zaidi ya kaya 300 kuunganishwa katika mfumo wa maji taka.

Akizungumza wakati wa kukagua utekelezaji wa mradi huo katika eneo la Kilimahewa, Waziri Kamwelwe amesema kuunganishwa kwa Kaya hizo kwenye mfumo wa maji taka kumeondoa tatizo la kutiririsha maji taka lililokuwa likichangia kuibuka kwa magonjwa ya milipuko mara kwa mara.

Wakati huohuo waziri huyo wakati akiwa jijini Mwanza amekabidhi magari matatu na pikipiki sita kwa Wilaya za Misungwi, Magu na Busega kwa ajili ya kuimarisha utekelezaji wa miradi ya maji safi inayoendelea kwenye Wilaya hizo.


Miradi ya Maji Safi pia inatekelezwa katika Miji ya Mwanza, Musoma na Bukoba ambapo inatarajiwa kugharimu kiasi cha fedha shilingi bilioni mia mbili na arobaini na tano ambazo zimetolewa na serikali ya Tanzania pamoja na wadau mbalimbali wa maendeleo.
WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI MHANDISI ISACK KAMWELWE AMESEMA SERIKALI IMEFANIKIWA KUTOKOMEZA MAGONJWA YA MILIPUKO. WAZIRI  WA  MAJI NA UMWAGILIAJI MHANDISI ISACK KAMWELWE AMESEMA SERIKALI IMEFANIKIWA  KUTOKOMEZA MAGONJWA  YA MILIPUKO. Reviewed by safina radio on November 29, 2017 Rating: 5

No comments