SHULE YA SEKONDARI YA KIMATAIFA YA MOSHI YA ISM MKOANI KILIMANJARO YATAKIWA KUWAPA MIKATABA WAFANYAKAZI WA SHULE HIYO.

2-11-2017

Naibu waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu sera, bunge,vijana,ajira na watu wenye ulemavu Mh Antony Mavunde ameuagiza uongozi wa shule ya sekondari ya kimataifa ya Moshi ISM iliyoko mkoani Kilimanjaro kuwapatia mikataba isiyokuwa na muda maalumu wafanyakazi wote wa shule hiyo kwa mujibu wa sheria.

Mh Mavunde ametoa maagizo hayo baada ya kutembelea shule hiyo na kubaini kuwa mikataba inayotolewa katika shukle hiyo kwa sasa iko kinyume cha sheria hivyo inahitaji kufanyiwa marekebisho.

Amesema kuwa ofisi yake itafuatilia suala hilo kwa karibu ili haki iweze kutendeka hasa kwa watanzania ambao wapo katika ajira ili waweze kupata ajira za kudumu zitakazowapa uhakika wa kuendesha maisha yao.


Awali wakitoa malalamiko yao kwa naibu waziri huyo wafanyakazi hao wamesema kuwa wanafanya kazi zao kwa hofu kutokana na kutokuwa na uhakika wa ajira za kudumu katika eneo lao la kazi.
SHULE YA SEKONDARI YA KIMATAIFA YA MOSHI YA ISM MKOANI KILIMANJARO YATAKIWA KUWAPA MIKATABA WAFANYAKAZI WA SHULE HIYO. SHULE YA  SEKONDARI  YA  KIMATAIFA  YA  MOSHI YA  ISM  MKOANI   KILIMANJARO  YATAKIWA  KUWAPA  MIKATABA WAFANYAKAZI  WA  SHULE  HIYO. Reviewed by safina radio on November 02, 2017 Rating: 5

No comments