WAKAZI WA MKOA WA ARUSHA WATAKIWA KUJITOKEZA KWA WINGI KUPIMA UGONJWA WA KISUKARI NA KUJUA NAMNA BORA YA KUJIKINGA

TAREHE 14-11-2017



Ikiwa leo ni siku ya maadhimisho ya siku ya kisukari duniani wakazi wa jiji la Arusha wametakiwa kujitokeza katika vituo mbalimbali vya afya ili kupata vipimo vya ugonjwa huo na namna ya kujikinga nao.

Ushauri huo umetolewa na mratibu wa magonjwa yasiyoambukiza mkoa wa Arusha Dr Rose Mende wakati akizungumza na waandishi wa habari katika maadhimisho ya siku ya ugonjwa wa kisukari duniani ambayo inafanyika leo,ambapo amesema kuwa huduma ya kupata huduma ya vipimo hivyo itatolewa katika wilaya zote za mkoa wa Arusha.

Dr Mende amesema kuwa huduma hiyo ya upimaji itatolewa bure kwa watu wote watakaojitokeza kwa siku ya  leo na  ya kesho,ambapo mbali na kutolewa kwa vipimo hivyo wataalamu wa afya pia watatoa elimu juu ya madhara na namna ya kukabilina na ugonjwa huo ambao umekuwa ukiwapata watu wengi bila kujali umri wao.

Amesema kuwa katika jiji la Arusha vituo vitakavyotumika kutoa huduma hiyo bure ni pamoja na hospitali ya mkoa ya Mount Meru,kituo cha Afya Levolosi na viwanja vya azimio la Arusha.


Hata hivyo maadhimisho ya siku ya ugonjwa wa kisukari duniani huadhimishwa kila ifikapo tarehe 14 Novemba ya kila mwaka ambapo kwa hapa Tanzania watu wenye ugonjwa huo ni asilimia 9.1 huku kauli mbiu ya mwaka huu ikiwa ni Wanawake na kisukari haki yetu kwa afya bora ijayo.
WAKAZI WA MKOA WA ARUSHA WATAKIWA KUJITOKEZA KWA WINGI KUPIMA UGONJWA WA KISUKARI NA KUJUA NAMNA BORA YA KUJIKINGA WAKAZI WA MKOA WA ARUSHA  WATAKIWA KUJITOKEZA KWA WINGI KUPIMA UGONJWA WA KISUKARI NA KUJUA NAMNA BORA YA KUJIKINGA Reviewed by safina radio on November 14, 2017 Rating: 5

No comments