WATU WAPATAO 28 WAMERIPOTIWA KUUAWA KATIKA MAANDAMANO NCHINI ERITREA

1-11-2017


Watu wapatao 28 wameripotiwa kuuawa na wengine 100 wamejeruhiwa katika maandamano yaliyofanyika kwenye mji mkuu wa Eritrea, Asmara.

Kundi kubwa la upinzani nchini humo la Red Sea Afar Democratic Oganization, limewaambia waandishi habari kuwa maandamano hayo yalikuwa makubwa  na kwamba watu kadhaa wamekamatwa.

Ubalozi wa Marekani nchini Eritrea umesema kuwa milio ya risasi ilisikika katika maeneo kadhaa mjini Asmara kutokana na maandamano hayo.

Mwanasiasa mmoja wa upinzani amesema serikali ya Eritrea ilijaribu kuidhibiti shule ya jumuia ya Waislamu, hatua iliyosababisha ghasia hizo.


Kiongozi wa muda mrefu wa Eritrea, Isaias Afewerki, ameitawala nchi hiyo tangu mwaka 1993, huku akiminya uhuru wa vyombo vya habari, kutofanyika kwa uchaguzi pamoja na kudhibitiwa kwa uhuru wa kidini.
WATU WAPATAO 28 WAMERIPOTIWA KUUAWA KATIKA MAANDAMANO NCHINI ERITREA WATU WAPATAO  28 WAMERIPOTIWA  KUUAWA KATIKA MAANDAMANO NCHINI ERITREA Reviewed by safina radio on November 02, 2017 Rating: 5

No comments