MKUU WA MAJESHI TANZANIA JENERALI VENANCE MABEO AMESEMA JESHI LA WANANCHI WA TANZANIA JWTZ LITATOA MAFUNZO YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA KWA ASKARI WAKE.

22-11-2017


Mkuu wa majeshi Tanzania Jenerali Venance Mabeo amesema Jeshi la Wananchi wa Tanzania JWTZ limejidhatiti kuhakikisha linatoa  mafunzo kwa askari wake kuhusu maswala ya Sayansi na Teknolojia katika kukabiliana na changamoto za ulinzi na usalama.

Jenerali Mabeo ameyasema hayo wakati wa uzinduzi wa kutoa mafunzo ya shahada ya kijeshi yatakayotolewa na Chuo cha Kijeshi cha TMA cha Monduli cha Mkoani Arusha kwa kushirikiana na Chuo cha Uhasibu Mkoani Arusha.

Mkuu huyo wa Majeshi amesema kwa sasa dunia imepiga hatua katika Sayansi na Teknolojia hasa katika masuala ya ulinzi hivyo lazima jeshi la Tanzania liwe tayari kwa taaluma hiyo.

Aidha, Jenerali Mabeo ameongeza kuwa sayansi na teknolojia inahitaji elimu kubwa ambapo katika mapigano ya Medali yanatumia teknolojia ya kisasa hivyo jeshi linapaswa kusonga mbele na kwenda na wakati, ili jeshi lisiweze kubaki katika kupambana na vitisho vya sasa.


Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dk. Florence Turuka amesema mafunzo hayo yanaumuhimu mkubwa hasa katika kipindi hiki ambapo Dunia inakabiliwa na changamoto ya Ugaidi, mapambano ya dawa za kulevya pamoja na mazingira.
MKUU WA MAJESHI TANZANIA JENERALI VENANCE MABEO AMESEMA JESHI LA WANANCHI WA TANZANIA JWTZ LITATOA MAFUNZO YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA KWA ASKARI WAKE. MKUU WA MAJESHI TANZANIA JENERALI VENANCE MABEO AMESEMA JESHI LA WANANCHI WA TANZANIA  JWTZ LITATOA MAFUNZO  YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA  KWA ASKARI WAKE. Reviewed by safina radio on November 22, 2017 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.