EMMERSON MNANGAGWA AWAHUTUBIA WAFUASI WAKE NCHINI ZIMBABWE
TAREHE 23-11-2017
Mtu anayetarajia kuwa rais mpya wa Zimbabwe, Emmerson Mnangagwa
amerejea jana nchini mwake na kuhutubia
wafuasi wake waliojawa na furaha, akisema nchi hiyo inafungua ukurasa mpya wa
siasa zake.
Aidha, Mnangagwa amesifu namna jeshi lilivyosimamia mchakato wa kumuondoa
madarakani mtangulizi wake Robert Mugabe kwa amani na utulivu, na kusema
kinachoshuhudiwa nchini Zimbabwe ni mwanzo wa demokrasia kamili.
Hali kadhalika ameinyoshea mkono
jumuiya ya kimataifa akisema Zimbabwe inahitaji msaada katika kukarabati uchumi
wake ulioporomoka.
Emmerson Mnangagwa alikuwa mshirika wa muda mrefu wa Rais Robert Mugabe, na
anatuhumiwa kuhusika na utekelezaji wa visa vingi vya uhalifu, yakiwemo mauaji
ya maelfu ya watu wakati wa makabiliano baina ya Mugabe na wapinzani wake wa kisiasa
mnamo miaka ya 1980.
Hata hivyo Mnangagwa anatarajiwa kukamilisha muhula wa Rais Mugabe hadi
uchaguzi mkuu utakapofanyika mwaka ujao,ambapo Wabunge wa upinzani ambao
wanasema chaguzi zilizopita zilikuwa na wizi wa kura, wametaka uchaguzi ujao
uwe huru na wa uwazi
EMMERSON MNANGAGWA AWAHUTUBIA WAFUASI WAKE NCHINI ZIMBABWE
Reviewed by safina radio
on
November 23, 2017
Rating:

No comments