TANZANIA YAUNGANA NA NCHI NYINGINE ULIMWENGUNI KUADHIMISHA SIKU YA WAFANYAKAZI MEI MOSI
Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mh
John Magufuli amewaongoza Watanzania katika maadhimisho ya sikukuu ya
wafanyakazi yanayofanyika leo duniani kote.
Hapa nchini maadhimisho hayo yamefanyika
kitaifa katika uwanja wa Samora mkoani Iringa,ambapo wafanyakazi waliandamana
wakiwa na mabango yenye jumbe mbalimbali zinazohusiana na sikukuu ya
wafanyakazi Mei Mosi.
Akizungumza
katika maadhimisho hayo Waziri wa Ofisi ya Waziri MKuu Sera Bunge Kazi na Watu
wenye Ulemavu Mh. Jenista Mhagama amesema kuwa ushirikiano baina ya Vyama vya
wafanyakazi pamoja na serikali ni lazima katika kuleta mabadiliko na kuendeleza
maisha ya wafanyakazi.
Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Iringa Bi Amina Masenza
amesema kuwa mkoa wa Iringa umekuwa ukiunga mkono juhudi zinazofanywa na
serikali katika kukuza uchumi wake kwa njia ya viwanda.
Katika maadhimisho hayo yalihudhuriwa na
viongozi mbalimbali akiwemo waziri mkuu Mh Majaliwa Kassimu Majaliwa,Spika wa
bunge Job Ndugai,mawaziri na viongozi wengine wa kiasiasa na wa dini.
Hata hivyo kauli mbiu ya maadhimisho ya Mei
Mosi mwaka huu ni kuunganishwa kwa mifuko ya Hifadhi ya jamii kulenge
kuboreshwa kwa mafao ya wafanyakazi.
TANZANIA YAUNGANA NA NCHI NYINGINE ULIMWENGUNI KUADHIMISHA SIKU YA WAFANYAKAZI MEI MOSI
Reviewed by safina radio
on
May 01, 2018
Rating:
No comments