SERIKALI KUENDELEA KUJENGA MAHAKAMA NCHINI.


 Ili kuhakikisha kuwa huduma za mahakama zinasogezwa karibu na wananchi serikali imesema kuwa itaendelea kujenga mahakama hizo kadri hali ya kifedha itakavyoruhusu.

Image result for PICHA YA ANTHONY MAVUNDE
MH.MAVUNDE

Hayo yameelezwa na naibu waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu Mh Antony Mavunde wakati akijibu maswali ya wabunge bungeni jijini Dodoma waliotaka kujua serikali ina mpango gani wa kujenga mahakama za mwanzo hapa nchini ili kusogeza huduma za kimahakama karibu na wananchi.

Mh Mavunde amesema kuwa kwa sasa kuna upungufu wa mahakama za mwanzo elfu tatu mia tatu na nne hapa nchini na kutokana na upungufu huo serikali imepanga kujenga mahakama hizo na kukarabati zingine kadri bajeti itakavyoruhusu.
                           
Hata hivyo bunge la bajeti linaendelea jijini Dodoma ambapo wabunge wanaendelea kujadili bajeti ya wizara ya viwanda na biashara kwa mwaka wa fedha wa 2018/2019 .

SERIKALI KUENDELEA KUJENGA MAHAKAMA NCHINI. SERIKALI KUENDELEA KUJENGA MAHAKAMA NCHINI. Reviewed by safina radio on May 11, 2018 Rating: 5

No comments