ZAIDI YA WALIMU 10,000 WAPO KATIKA MPANGO WA KUAJIRIWA NA SERIKALI ILI KUPUNGUZA CHANGAMOTO ZA SEKTA YA ELIMU NCHINI.


Ili kupunguza upungufu wa waalimu wa shule za msingi hapa nchini serikali imesema kuwa ina mapango wa kuwaajiri waalimu zaidi ya elfu kumi ifikapo mwezi Juni mwaka huu.

Image result for naibu waziri wa nchi ofisi ya rais tawala za mikoa na serikali za mitaa TAMISEM Mh Joseph Kakunda

Hayo yameelezwa na naibu waziri wa nchi ofisi ya rais tawala za mikoa na serikali za mitaa TAMISEM Mh Joseph Kakunda wakati akijibu maswali ya nyongeza leo bungeni jijini Dodoma,ambapo wabunge walitaka kujua ni lini serikali itaondoa changamoto mbalimbali zinazokabili sekta ya elimu ikiwemo upungufu wa waalimu.

Amesema kuwa kwa sasa kinachofanyika ni baraza la mitihani hapa nchini NECTA  kukagua na kuchambua vyeti vya waalimu walioomba nafasi hizo na watakaochaguliwa watasambazwa katika maeneo mbalimbali hapa nchini.

Aidha katika hatua nyingine Mh Kakunda amesema kuwa serikali pia imetenga kiasi cha shilingi milioni mia tano kwa ajili ya kujenga vyoo na nyumba za waalimu katika maeneo mbalimbali hapa nchini lengo likiwa ni kuondoa changamoto zinazowakabili waalimu pamoja na wanafunzi.

Bunge la bajeti linaendelea mjini Dodoma ambapo wabunge wanaendelea kujadili bajeti ya wizara ya elimu,sayansi tekinolojia na mafunzo ya ufundi kwa mwaka wa fedha wa 2018/2019  iliyowasilishwa hapo juzi na waziri wa wizara hiyo Mh Joyce Ndalichako.

ZAIDI YA WALIMU 10,000 WAPO KATIKA MPANGO WA KUAJIRIWA NA SERIKALI ILI KUPUNGUZA CHANGAMOTO ZA SEKTA YA ELIMU NCHINI. ZAIDI YA WALIMU 10,000 WAPO KATIKA MPANGO WA KUAJIRIWA NA SERIKALI ILI KUPUNGUZA CHANGAMOTO ZA SEKTA YA ELIMU NCHINI. Reviewed by safina radio on May 02, 2018 Rating: 5

No comments