NCHI MBALIMBALI ZATAKIWA KUJENGA MFUMO BORA WA BIASHARA


Mwenyekiti wa Shirika la Fedha Duniani IMF, Bi Christine Lagarde amesema nchi mbalimbali zinatakiwa kujenga mfumo bora wa biashara ya kimataifa ili kukabiliana na changamoto za mageuzi ya kidijitali katika sekta ya biashara.

Image result for PICHA YA CHRISTINE LAGARDE RAIS WA IMF
BI LAGARDE

Bi Lagarde pia amesema, ubora wa uchumi wa dunia unategemea mzunguko mzuri wa biashara, na kusema kuwa katika siku za karibuni, ongezeko la biashara limesukuma mbele maendeleo ya uchumi wa dunia lakini, mfumo wa kujilinda kibashara unaoendelea kujitokeza umezuia mwelekeo huu mzuri.

Mwnyekiti huyo,amesema hivi sasa biashara bora inategemea biashara zaidi ya huduma, ongezeko la kiwango cha uzalishaji na ushirikishi mzuri zaidi.

Ametoa wito kwa nchi mbalimbali kupinga mfumo wa kujilinda kibiashara, na kuondoa vitendo visivyokuwa na usawa vya biashara ili kujenga mazingira ya kibiashara yenye usawa


NCHI MBALIMBALI ZATAKIWA KUJENGA MFUMO BORA WA BIASHARA NCHI MBALIMBALI ZATAKIWA KUJENGA MFUMO BORA WA BIASHARA Reviewed by safina radio on May 15, 2018 Rating: 5

No comments