USTAWI WA JAMII NCHINI INAKABILIWA NA CHANGAMOTO YA UPUNGUFU WA WATAALAMU WANAOPASWA KUHUDUMIA JAMII.


Imeelezwa kuwa sekta ya Ustawi wa Jamii nchini inakabiliwa na changamoto ya upungufu wa wataalamu wanaopaswa kuhudumia jamii kuanzia ngazi ya mitaa, vijiji, Kata na Halmashauri ambapo kwa sasa mahitaji ni elfu 23 huku wataalam waliopo ikiwa ni 730 katika Halmashauri zote nchini.
Hayo yameelezwa na Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa wana Taaluma wa Ustawi wa Jamii nchini (TASWO) Bw Awadh Mohamed katika mkutano wa uchaguzi wa viongozi wa TASWO mkoa wa Manyara uliofanyika  wilayani Babati.

Amesema  kuwa watoa huduma za ustawi wa jamii ni wachache kwani wanaotakiwa ni elfu ishirini na tatu lakini waliopo kwa sasa ni 730 katika Halmashauri zote nchini huku wakiwa hawakidhi mahitaji ya jamii katika kutatua matatizo mbalimbali yakiwemo ya  familia, mtu mmoja mmoja na makundi yenye mgawanyiko.
Kwa upande wake Mwenyekiti mpya wa TASWO Mkoa wa Manyara Ezekiel Assecheck amesema kufunguliwa kwa tawi hilo mkoani humo kutasaidia kuandaa mipango mikakati ya utoaji wa ushauri kwa Serikali na watoa huduma katika kuibua changamoto mbalimbali zilizopo katika maeneo yao.
 Naye mjumbe wa bodi ya TASWO Taifa, Songoro Msongo amewataka wanachama na viongozi waliochaguliwa kushirikiana, kwani kila mtu ni wa muhimu  katika kutoa mchango wake katika umoja huo na kuweza kusonga mbele.

USTAWI WA JAMII NCHINI INAKABILIWA NA CHANGAMOTO YA UPUNGUFU WA WATAALAMU WANAOPASWA KUHUDUMIA JAMII. USTAWI WA JAMII NCHINI INAKABILIWA NA CHANGAMOTO YA UPUNGUFU WA WATAALAMU WANAOPASWA KUHUDUMIA JAMII. Reviewed by safina radio on May 23, 2018 Rating: 5

No comments