MTOTO AUAWA KWA KUKATWA KICHWA NCHINI MALI.
Watu waliokuwa na silaha wamemuua kwa kumkata kichwa mtoto
wa miaka mitano mwenye ulemavu wa ngozi albino nchini Mali.
Mtoto aliyefahamika kwa jina la Djeneba Diarra, aliibiwa na
watu hao usiku wa manane wakati akiwa amelala nyumbani kwao pamoja na mama yake
na dada yake, katika kijiji cha Fana nchini humo.
Mama mzazi mtoto huyo ameushuhudia mkasa huo akisema kuwa
alijaribu kuwakimbiza watu hao waliomchukua mwanawe lakini baadae alirudi nyuma
ili kumlinda mtoto wake mwingine ambaye pia ni albino.
Polisi nchini humo wamesema wanahofia kuwa mauaji hayo yalikuwa
ni mauaji ya kishirikina na uchawi unaotegemea viungo vya albino ambapo Wengi
wanauawa kwa kukatwa viungo vyao vya mwili,vinavyotumika katika uchawi
unaoaminiwa kuleta utajiri na mafanikio katika maisha jambo ambalo sii kweli.
Kwa kipindi cha nyuma
mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi yalikuwa ni tatizo kubwa katika nchi
kadhaa za Kiafrika ikiwa ni pamoja na Malawi, Msumbiji,Tanzania na Zimbabwe
pamoja na mataifa mengine ya Afrika Magharibi.
MTOTO AUAWA KWA KUKATWA KICHWA NCHINI MALI.
Reviewed by safina radio
on
May 16, 2018
Rating: 5
Support
Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.
No comments