FATOU BENSOUDA AKAMILISHA ZIARA YAKE DRC
Mwendesha mashtaka wa mahakama ya Kimataifa ya ICC Fatou
Bensouda amekamilisha ziara yake nchini DRC ambako amekutana na watu mbali
mbali akiwemo rais Joseph Kabila.
FATOU BANSOUDA. |
Fatou Bensouda,
alikutana na Joseph Kabila huko Kinshasa, ambapo walijadili vurugu katika DRC, hali ya mahakama
ya kitaifa na ushirikiano kati ya Ofisi ya ICC na DRC.
Bensouda pia
alikutana na bazara la maaskofu,
upinzani, wanasheria na mashirika ya kiraia na kuulizia hali ya haki za binadamu.
Kwa mujibu wa Fatou Bensouda, serikali ina jukumu la msingi
la kuanzisha kesi za kisheria dhidi ya wahalifu wa ukiukwaji wa haki za
binadamu nchini DRC kwa lengo la kukomesha kutokujali na kurejesha hali ya haki
na amani nchini.
Kwa upande wake, Mwanasheria Mkuu wa Jamhuri ya Kidemocratia
ya Congo, Flory Kabange Numbi, alimhakikishia Mwendesha Mashitaka wa ICC uamuzi
wa mamlaka za Kinshasa kuchunguza kesi za ukiukwaji wa haki za binadamu na
kufungua mashitaki dhidi ya wahalifu hao.
Hata hivyo Mnamo Machi 2016, afisa mkuu wa ICC Margot
Tedesco, alisema kuwa Mahakama ya ICC tayari imepokea taarifa kuhusu mauaji
huko Beni, Kivu kaskazini .
FATOU BENSOUDA AKAMILISHA ZIARA YAKE DRC
Reviewed by safina radio
on
May 04, 2018
Rating:
No comments