RAIS MAGUFULI AWATAKA WATANZANIA KUITUNZA AMANI.


Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh John Magufuli amewataka watanzania kuendelea kuitunza na kuilinda amani iliyoko hapa nchini kwani palipo na amani ndipo penye maendeleo.

Image result for PICHA RAIS MAGUFULI
RAIS MAGUFULI
Mh Magufuli ametoa kauli hiyo leo wakati akizungumza na wananchi wa eneo la Ilula mkoani Iringa akiwa njiani kuelekea mkoani Morogoro,ambapo amesema kuwa Tanzania imejengwa katika misingi ya upendo na amani hivyo ni vyema Watanzania wakaienzi misingi hiyo bila kujali makabila yao.

Ameongeza kuwa kukiwa na amani wawekezaji kutoka nje ya nchi watakuja kuwekeza hapa nchini na uchumi wa Tanzania utakuwa kwa kasi,huku akiwataka wananchi kuwapuuza wale wote wanaotaka kuleta vurugu hapa nchini kwa kurubuniwa kwa njia mbalimbali na watu wasioitakia mema Tanzania.

Aidha akiwa katika eneo la Ruaha Mbuyuni rais Magufuli aliweza kukabidhi kiasi cha shilingi milioni tano kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya 

Ruaha,ambapo amesema kuwa serikali ya awamu ya tano itaendelea kuboresha sekta ya afya kwa kutenga bajeti zaidi katika wizara ya afya.
Hata hivyo rais Mgufuli ameondoka mkoani Iringa,na kwa sasa yupo mkoani Morogoro ambapo atazindua ujenzi wa barabara ya Kidatu hadi Ifakara.

RAIS MAGUFULI AWATAKA WATANZANIA KUITUNZA AMANI. RAIS MAGUFULI AWATAKA WATANZANIA KUITUNZA AMANI. Reviewed by safina radio on May 04, 2018 Rating: 5

No comments