TATIZO LA AJIRA KWA VIJANA LAENDELEA.
MKUU WA WILAYA YA BABATI RAYMOND MUSHI. |
Amesema ajira zitaongezeka endapo
uchumi utakuwa,yaani shughuli za uzalishaji mali na utoaji wa huduma na
shughuli zote hizo zinategemea kuongezeka kwa Uwekezaji kwani bila uwekezaji
kuongezeka hakutokuwa na ongezeko la ajira kwa Vijana.
Mkuu huyo ameongeza kuwa serikali
iliona tatizo la ajira kuwa kubwa ndio maana imejipanga kuondoa
tatizo la ajira kwa kutekeleza ilani ambazo zinalenga kuwezesha nchi ya
Tanzania kuwa na uchumi wa kati inayoongozwa na viwanda.
Kwa upande wake mmoja wa mmiliki wa
kiwanda cha Mati Super Brand Bw Gasper Mlay amesema kuwa ili Tanzania iweze
kuendelea inawapasa kulipa kodi ili kuweza kujenga Barabara bora, kununua
madawa hospitalini na maji safi,kwani hivyo vyote vikikosekana hata
mfanyabiashara hatoweza kufanya biashara vizuri.
TATIZO LA AJIRA KWA VIJANA LAENDELEA.
Reviewed by safina radio
on
May 04, 2018
Rating:
No comments