MALORI MAWILI YAKAMATWA LONGIDO


Mamlaka ya mapato Tanzania TRA Mkoa wa Arusha imekamata malori mawili katika eneo la Longido yaliyokuwa yakisafirisha bidhaa za sukari pamoja na mafuta ya kupikia kinyume na sheria zenye kugharimu fedha zaidi ya shilingi milioni 20.

Image result for PICHA YA CHARLES KICHERE
BW KICHERE.

Akitoa taarifa hiyo kwa waandishi wa habari Kamishna Mkuu wa Mapato Tanzania Charles Kichere amesema kuwa usiku wa kuamkia tarehe 11 katika maeneo ya Longido gari lenye namba za uasjili T 985 AJP na T 840 ABFyalikamatwa yakiwa yamepakia bidhaa za magendo.

Amesema kuwa Katika uchunguzi uliofanyika ulibaini kuwepo kwa bidhaa mbalimbali ambapo katika lori la kwanza kulikuwa na mifuko 193 ya sukari yenye ujazo wa kilo 50 kila mmoja huku katika lori la pili kukiwa na mifuko 169 ya sukari yenye ujazo wa kilo 50 kila mmoja, maboksi 40 ya mafuta ya kupikia aina ya Karibu yaliyofungwa kwa ujazo tofauti.

Amesema kuwa katika boksi hizo kulikuwepo na kopo 24 zenye ujazo wa nusu lita kila moja,makopo 12 yenye ujazo wa kilo mbili kila moja, makopo 12 yenye ujazo wa kilo moja kila moja,boksi 3 za mafuta ya kupikia aina ya Daria yenye makopo 12 kwa ujazo wa kilo moja kwa kila moja.

Aidha kamishna huyo amesema kuwa jumla ya thamani ya bidhaa hizo ni zaida ya shilingi milioni 20 ambapo kodi ya bidhaa hizo ni zaidi ya shilingi milioni 28 huku adhabu na faini ya bidhaa hizo ikiwa ni zaidi ya shilingi milioni 10 na kufanya jumla kuu ya mapato yanayotakiwa kulipwa serikalini kufikia zaidi ya shilingi milioni 39.


MALORI MAWILI YAKAMATWA LONGIDO MALORI MAWILI YAKAMATWA LONGIDO Reviewed by safina radio on May 16, 2018 Rating: 5

No comments