MASHAMBULIZI YATISHIA SEKTA YA UTALII AFRIKA YA KUSINI
Wabunge
wa Afrika Kusini wameonya kuwa mashambulizi dhidi ya watalii nchini humo
yanatishia sekta ya utalii, ambayo imekuwa kichocheo kikubwa cha ukuaji wa
uchumi katika nchi hiyo.
Kauli
hiyo imetolewa baada ya watalii watatu wa Ujerumani kuporwa mali zao Jumapili
na watu wanne katika eneo la Ballito, karibu na mji wa Durban, mashariki mwa
Afrika Kusini.
Watalii
hao wamekumbwa na shambulizi hilo wakati wakielekea katika uwanja wa ndege wa
King Shaka, lakini hakuna mtu aliyejeruhiwa.
Kaimu
mwenyekiti wa kamati ya uwekezaji na utalii ya bunge la Afrika Kusini Bi Lusizo
Makhubele-Mashele amesisitiza kuwa tishio lolote la kiusalama kwenye sekta
hiyo, litaleta athari mbaya.
Bi Lusizo ametoa wito kwa idara za utekelezaji
wa sheria ziwafikishe wahalifu hao mbele ya sheria haraka iwezekanavyo.
MASHAMBULIZI YATISHIA SEKTA YA UTALII AFRIKA YA KUSINI
Reviewed by safina radio
on
May 15, 2018
Rating:
No comments