UBAELGIJI YAELEZA SABABU YAKUMUITA BALOZI WAKE KUTOKA CONGO DRC.
Serikali ya Ubelgiji imeeleza sababu za
kumuita balozi wake nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya congo tangu mwezi January
mwaka huu, baada ya nchi hiyo kuwa na mahusiano mabaya ya kidiplomasia na
serikali ya kinshasa.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Ubelgiji Didier
Reinders alithibitisha Jumatatu wiki hii uamuzi wa Brussels wa kumrejesha
nyumbani balozi wake aliyekuwa jijini Kinshasa Bertrand de Crombrugghe,
akieleza kuwa mazingira ya mahusiano ya kidiplomasia kati ya mataifa hayo
mawili hayakuwa mazuri huku akiishutumu serikali ya DRC kushindwa kuonyesha
ushirikiano katika masuala mengi ikiwemo ya kijeshi lakini pia kisiasa.
Hata hivyo vyombo vya habari vya Ubelgiji hali
kadhalika vyanzo vya kidiplomasia vimeripoti kuwa kulikuwa na uvunjaji wa
uaminifu kati ya nchi hiyo ambayo iliitawala kikoloni DRC na serikali ya
Kinshasa baada ya kutangazwa uamuzi wa kufungwa kwa ubalozi mdogo wa shengen,
hatua ambayo ilionekana kuchochea uhasama zaidi.
Balozi Bertrand de Crombrugghe kwa upande wake
amesema kuwa Wizara ya mambo ya nje ya Ubelgiji ilishangazwa na hatua ya
Kinshasa baada ya yeye kupokea barua ya kumtaka aondoke nchini humo.
Ubelgiji imekuwa ikiitaka serikali ya Kinshasa
kuboresha mazingira ya kisiasa na kuhakikisha makubaliano yaliyosainiwa chini
ya upatanisho wa kanisa Katolijki CENCO yanatekelezwa, na uchaguzi unafanyika
chini ya misingi ya kidemokrasia nchini humo.
UBAELGIJI YAELEZA SABABU YAKUMUITA BALOZI WAKE KUTOKA CONGO DRC.
Reviewed by safina radio
on
May 01, 2018
Rating:
No comments