RAIS MAGUFULI AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA BANDARINI.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh John Magufuli leo amefanya ziara ya kushtukiza kwenye bandari ya Dar-es-salaam kukagua matenki ya mafuta ya kupikia kufuatia kuwepo kwa taarifa ya mafuta kuzuiliwa bandarini wakati wananchi wanahofia kupanda kwa bei ya mafuta hayo muda sii mrefu.

Image result for PICHA YA RAIS MAGUFULI


Mara baada ya Rais Magufuli kuwasili bandarini,kwanza alipokea maelezo ya Wataalam mbalimbali wanaohusika kulifatilia sakata hilo ambapo mmoja wa maafisa wa TRA ambaye alimwambia Rais kuwa kwenye taarifa ya mafuta iliyotolewa kuna udanganyifu.

Aidha Rais Magufuli amebaini kuwa baadhi ya makontena yaliyodaiwa kuwa na mafuta ghafi ya kupikia yalikuwa na mafuta masafi ambapo amesema kuwa baadhi ya wafanyabiashara wanatumia nafasi zao kuwalaghai wananchi na kutaka mafuta ghafi kutozwa bei ya juu ili kulinda viwanda vya ndani.

Hata hivyo amemtaka mkemia mkuu wa serikali kufanya kazi kwa kuzingatia taratibu na maadili na kuweka maslahi ya taifa mbele.

Wakati huohuo Rais Magufuli amempandisha cheo kamishina wa TRA bandari ya Dar es salaam Bw. Ben Usaje kuwa kamishina kamili wa TRA bandarini hapo kufuatia kusimamia vyema uchunguzi alioagiza ufanyike bandarini hapo.


RAIS MAGUFULI AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA BANDARINI. RAIS MAGUFULI AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA BANDARINI. Reviewed by safina radio on May 15, 2018 Rating: 5

No comments