SERIKALI YAZIAGIZA HALMASHAURI KUTOA FEDHA ZA MIKOPO KWA WANAWAKE, VIJANA,NA WENYE ULEMAVU.


Serikali imeziagiza Halmashauri zote Nchini kutoa fedha za mikopo ya asilimia kumi ya mapato yao kwa wanawake,vijana,na watu wenye ulemavu bila kuwatoza riba yoyote.

Image result for PICHA YA SULEIMANI JAFFO
MH. JAFFO.
Agizo hilo limetolewa jijini Dar es salaam na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa TAMISEMI Mh. Selemani Jaffo alipokuwa akizungumza na wafanyabiashara wa soko la Magomeni lengo likiwa ni kuzungumzia hatma ya wafanyabiashara wa soko hilo katika siku za usoni.


Takribani shilingi bilioni 9 zinatarajiwa kutumika katika ujenzi wa soko la Magomeni ikiwa ni mwendelezo wa serikali wa kuboresha masoko na vituo vya mbasi nchini ili zifanyekazi kwa ufanisi.




SERIKALI YAZIAGIZA HALMASHAURI KUTOA FEDHA ZA MIKOPO KWA WANAWAKE, VIJANA,NA WENYE ULEMAVU. SERIKALI YAZIAGIZA HALMASHAURI KUTOA FEDHA ZA MIKOPO  KWA WANAWAKE, VIJANA,NA WENYE ULEMAVU. Reviewed by safina radio on May 11, 2018 Rating: 5

No comments