SERIKALI IMESEMA INATAMBUA MCHANGO WA MWANA,KE.
Serikali imesema kuwa inatambua mchango wa
mwanamke kuanzia ngazi ya familia na taifa kwa ujumla na kwa sababu hiyo ndio
maana serikali imeziagiza halmashauri zote nchini kutenga asilimia kumi ya
mapato yake kwa ajili mikopo ya wanawake na vijana.
Hayo yamesemwa mapema leo bungeni jijini
Dodoma na naibu waziri wa fedha na mipango Mh. Dk. Ashantu Kijaji wakati
akijibu swali la mbunge wa viti maalum Mh. Bupe Mwakang’ata aliyetaka kujua ni lini
serikali itawawezesha wanawake kibenki hususani wanaoishi katika mikoa ya
pembezoni.
DK. KIJAJI. |
Hata hivyo bunge linaendelea jijini Dodoma
ambapo wabunge wanaendelea kujadili bajeti za wizara mbalimbali kwa mwaka wa
fedha 2018/2019.
SERIKALI IMESEMA INATAMBUA MCHANGO WA MWANA,KE.
Reviewed by safina radio
on
May 16, 2018
Rating:
No comments