RAIS TRUMP KUPUNGUZA IDADI YA WANAJESHI KOREA KUSINI
Rais
wa Marekani Donald Trump ameigaiza wizara ya ulinzi nchini humo kujitayarisha
kupunguza idadi ya wanajeshi wa Marekani walioko nchini Korea Kusini.
RAIS TRUMP WA MAREKANI |
Gazeti
la Marekani la New York Times limeripoti kuwa kupunguzwa kwa idadi ya wanajeshi
hao hakulengi kuwa mojawapo ya vigezo kuelekea mkutano wa kilele kati ya Trump
na kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un.
Kutokana na makubaliano ya amani kati ya Korea
Kusini na Kaskazini huenda yakapunguza haja ya kuwepo wanajeshi zaidi ya elfu
ishirini na tatu wa Marekani katika rasi
ya Korea.
Mahusiano
kati ya Korea mbili yameimarika hasa baada ya Korea Kaskazini kutangaza mwezi
uliopita kuwa itaachana na mpango wake wa kinyuklia na viongozi wa nchi hizo
mbili kukutana kwa mkutano wa kihistoria.
RAIS TRUMP KUPUNGUZA IDADI YA WANAJESHI KOREA KUSINI
Reviewed by safina radio
on
May 04, 2018
Rating:
No comments