ZAIDI YA VYUO VIKUU 20 AFRIKA ZATARAJIA KUINGIZA MITAALA YA KILIMO HIFADHI.


ARUSHA.

Zaidi ya vyuo vikuu vya kilimo 20 barani Afrika vinatarajia kuingiza mitaala ya kilimo hifadhi katika vyuo vyao ili kuwawezesha maafisa ugani wanaohitimu katika vyuo hivyo kupata elimu ya kilimo hicho na baadaye kuwafikishia wakulima ambao bado hawajafikiwa na elimu ya kilimo hifadhi.


Hayo yameelezwa na mkurugenzi mtendaji wa shirika la kilimo hifadhi barani Afrika Bw Saidi Mkomwa alipokuwa akizungumza katika semina ya wadau wa matrekta ya kuwaonesha namna ya kutumia trekta katika kilimo hifadhi iliyofanyika jijini Arusha.

Bw  Mkomwa amesema kuwa katika uhamasishaji wa wakulima juu ya kulima kilimo hifadhi shirika hilo tayari limewakutanisha watoa elimu wa  vyuo vikuu vya kilimo  ili kuangalia namna ya kuingiza mitaala hiyo  ili kilimo hifadhi kifundishwe katika vyuo hivyo kwa lengo la kuwezesha wahitimu kupata utaalamu wa kuwaelekeza wakulima huko waendako.

Ameongeza kuwa  hadi sasa Tanzania  inalima hekta elfu 30 za kilimo hifadhi huku kiwango hicho kikiwa ni cha chini kuliko nchi za bara la Afrika ambapo idadi hiyo inatokana na ukosefu wa elimu kwa wakulima juu ya  kulima kilimo  hifadhi ambacho kwa sasa ndicho kilimo  chenye tija kwani uzalishaji wake ni mkubwa zaidi kuliko kilimo cha mazoea.

Hata hivyo amesema kuwa wanaendelea kushirikiana na shirika la kilimo hifadhi tanzania ili kutoa elimu ya kutosha kwa wakulima na kuwasaidia wadau kuachana na kilimo cha kawaida na kulima kilimo hifadhi .

ZAIDI YA VYUO VIKUU 20 AFRIKA ZATARAJIA KUINGIZA MITAALA YA KILIMO HIFADHI. ZAIDI YA VYUO VIKUU 20 AFRIKA ZATARAJIA KUINGIZA MITAALA YA KILIMO HIFADHI. Reviewed by safina radio on May 23, 2018 Rating: 5

No comments