VIWANDA VYA SARUJI VINACHANGAMOTO YA KUTOKUWA NA MIUNDOMBINU YA KUDHIBITI VUMBI KATIKA VIWANDA VYA SARUJI NA CHOKAA.
Imeelezwa kuwa viwanda vya saruji na
chokaa vilivyoko mkoani Tanga vinakabiliwa na changamoto ya kutokuwa na
miundombinu thabiti ya kudhibiti vumbi kutoka viwandani hali inayochangia
uchafuzi wa mazingira na migogoro kwa wananchi.
Hayo
yamesemwa na katibu tawala wa mkoa huo Bi Anuciata Lyimo alipokuwa akizungumza
na waandishi wa habari kuhusiana na jinsi ambavyo wamekuwa wakikabiliana na
utunzaji wa mazingira mkoani humo.
Amesema kuwa pamoja na kuendelea kutoa elimu ya utunzaji mazingira lakini bado
viwanda vya saruji na chokaa vinakabiliwa na changamoto ya kudhibiti vumbi
kutoka viwandani hali inayochangia uchafuzi wa mazingira.
Aidha ameongeza kuwa katika sekta ya mazingira bado baadhi
ya viwanda ikiwemo cha Korona cha kuchakata mkonge hutiririsha maji taka kwenye
vyanzo vya maji hivyo kuhatarisha afya za watumiaji wengine wa maji.
Hata hivyo amesema kuwa pamoja na kuwa mafanikio mbali mbali
yamepatikana katika utekelezaji wa sheria ya mazingira bado wanaendelea
na Ukaguzi wa Usafi wa Mazingira kwa ngazi ya kata na Vijiji na kufuata
Usimamizi wa agizo la kufanya usafi wa mazingira kwa kila jumamosi ya mwisho wa
mwezi ili kudhibiti changamoto hizo.
VIWANDA VYA SARUJI VINACHANGAMOTO YA KUTOKUWA NA MIUNDOMBINU YA KUDHIBITI VUMBI KATIKA VIWANDA VYA SARUJI NA CHOKAA.
Reviewed by safina radio
on
May 02, 2018
Rating:
No comments