SERIKALI KUENDELEA KUWEKA MIKAKATI YA KUTATUA CHANGAMOTO ZINAZOWAKABILI VIJANA NCHINI


Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge Kazi Vijana Ajira na Wenye Ulemavu Anthon Mavunde amesema kuwa serikali inaendelea kuweka mikakati ya kutatua changamoto zinazowakabili vijana ili kuhakikisha wanapata ajira.

Image result for PICHA YA ANTONY MAVUNDE
MH. ANTHON MAVUNDE
Mh. Mavunde ameyasema hayo wakati akifungua Kongamano Kivuli la Vijana wa Umoja wa Mataifa jijini Dodoma lililowakutanisha vijana kutoka nchi mbali mbali kujadili changamoto zinazowakabili vijana Duniani ili kuzipatia ufumbuzi.

Aidha, amesema kuwa serikali ya Tanzania imedhamiria  kumkwamua kijana wa kitanzania hasa katika kumpatia ujuzi stahiki ambapo ofisi ya Waziri Mkuu inaendesha mafunzo kupitia  Programu ya Ukuzaji Ujuzi ya Miaka Mitano.

Mh. Mavunde amebainisha kuwa Mpango huo wa Programu ya Miaka mitano inalenga kuwafikia vijana Milioni nne na Laki nne kwa ajili ya kulenga vijana wote wawe na ujuzi stahiki katika dunia ya leo.

Hata hivyo Naibu Waziri Mavunde amewataka vijana kutumia mitandao ya kijamii kutafuta fursa za kimaendeleo.





SERIKALI KUENDELEA KUWEKA MIKAKATI YA KUTATUA CHANGAMOTO ZINAZOWAKABILI VIJANA NCHINI SERIKALI KUENDELEA KUWEKA MIKAKATI YA KUTATUA CHANGAMOTO ZINAZOWAKABILI VIJANA NCHINI Reviewed by safina radio on May 01, 2018 Rating: 5

No comments