ZAIDI YA WATU 60 WAUAWA KATIKA JIMBO LA ADAMAWA, NIGERIA.
Watu zaidi ya 60 wameuawa katika jimbo la Adamawa, Kaskazini
Mashariki mwa Nigeria baada ya kutokea kwa mashambulizi mawili ya bomu
yaliyolenga msikiti na soko.

Licha ya kuwa hakuna mtu au kundi ambalo limedai kuhusika na
mashambulizi hayo, mji wa Mubi katika jimbo la Adamawa kaskazini mashariki mwa
Nigeria, umekua ukilengwa na mashambulizi ya mara kwa mara ya Boko Haram,ambapo
mnamo mwezi Novemba mwaka uliopita, watu 50 waliuawa katika mashambulizi ya
awali.
Hata hivyo maafisa wa usalama wanasema mashambulizi hayo ya
kujitoa mhanga, yalitekelezwa na wavulana wadogo waliotumwa na kundi la Boko
Haram.
Waathirika wote walipelekwa katika hospitali nne tofauti katika
mji wa Mubi na maeneo jirani.
Aidha mauaji hayo yametokea siku moja tu baada
ya Rais Donald Trump wa Marekani kukutana na kufanya mazungumzo
katika ikulu ya White House na Rais Muhammadu Buhari wa Nigeria na kuahidi
kuisaidia nchi hiyo ya magharibi mwa Afrika katika kupambana na makundi ya
wabeba silaha.
ZAIDI YA WATU 60 WAUAWA KATIKA JIMBO LA ADAMAWA, NIGERIA.
Reviewed by safina radio
on
May 02, 2018
Rating:
No comments