TRUMP KUKUTANA NA KIM JONG UN JUN 12 NCHINI SINGAPORE.


Rais wa Marekani, Donald Trump amesema atakutana na kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong Un Juni 12 nchini Singapore.

Image result for PICHA YA TRUMP
RAIS TRUMP.
Mkutano huo wa kilele utakuwa wa kihistoria na wa aina yake kati ya viongozi hao wawili ambapo Trump ameandika katika ukurasa wake wa Twitter kwamba watajitahidi kuufanya mkutano huo uwe wa muhimu kwa ajili ya amani ya dunia.

Viongozi hao wawili wanatarajia kujadiliana kuhusu maendeleo ya silaha za nyuklia za Korea Kaskazini pamoja na majaribio yake ya makombora ambayo yamesababisha mvutano wa muda mrefu kati ya Marekani na Korea Kaskazini.

Image result for PICHA YA KIM JONG UN
RAIS WA KOREA KASKAZINI KIM JONG UN
Tangazo hilo la Trump limetolewa muda mchache baada ya raia watatu wa Marekani waliokuwa wamefungwa gerezani Korea Kaskazini kuwasili Marekani, baada ya kuachiwa huru na utawala wa Kim.

Trump amesema atafurahi kama watafanikiwa kuhakikisha hakuna kabisa silaha za nyuklia katika Rasi ya Korea.









TRUMP KUKUTANA NA KIM JONG UN JUN 12 NCHINI SINGAPORE. TRUMP KUKUTANA NA KIM JONG UN JUN 12 NCHINI SINGAPORE. Reviewed by safina radio on May 11, 2018 Rating: 5

No comments