WATU ZAIDI YA 40 WAFARIKI NCHINI KENYA


Zaidi ya watu 40 wamefariki na maelfu ya wengine kuachwa bila makazi wakati bwawa moja mjini Nakuru nchini Kenya lilipovunja kuta zake Jumatano usiku.
Jitihada za kutafuta miili ya watu waliokufa inaendelea
Shirika la kupambana na majanga nchini Kenya linasema kuwa hadi sasa watu wengi hawajulikani waliko ambapo Maafisa wa uokozi kutoka mashirika tofauti nchini humo wanaendelea na jitihada za kutafuta miili ya watu waliokufa kutokana na mkasa huo.
Eneo hilo la Solai katika kaunti ya Nakuru nchini Kenya, lina mabwawa saba yanayotumika katika kilimo cha umwagiliaji.
Waziri wa mambo ya ndani wa  Kenya Fred Matiang'i amesema serikali imeanzisha uchunguzi kubaini uthabiti wa mabwawa mengine sita yaliosalia.
Mapema leo Ijumaa kulikuwa na hisia ya wasiwasi baada ya taarifa kusambaa katika mitandao ya kijamii kwamba bwawa la pili limepasuka katika eneo hilo.

WATU ZAIDI YA 40 WAFARIKI NCHINI KENYA WATU ZAIDI YA 40 WAFARIKI NCHINI KENYA Reviewed by safina radio on May 11, 2018 Rating: 5

No comments