WAKULIMA WATAKIWA KUFUATA USHAURI UNAOTOLEWA NA WATAALAM


Wakulima hapa nchini wametakiwa kufuata ushauri unaotolewa na wataalamu wa kilimo ili waweze kufahamu namna ya kukabiliana na changamoto mbalimbali ikiwemo magonjwa yanayoshambulia mazao yao.

Image result for PICHA YA MAHINDI NA MAHARAGE


Ushauri huo umetolewa na afisa ugani wa mtandao wa vikundi vya wakulima Tanzania mkoa wa Manyara Bw Donald Laizer wakati akizungumza na Redio Safina kuhusu magonjwa mbalimbali yanayoshambulia zao la mahindi na maharage mkoani humo.

Amesema kuwa kutokana na wakulima wengi kutofuata ushauri unaotolewa na wataalamu wameshindwa kujua namna ya kupambana na magonjwa hayo haswa ugonjwa wa kutu unaosababisha mahindi na maharage kunyauka.
                       
Kwa upande wa wakulima wa kijiji cha Gedemara kata ya Galapo mkoani Manyara wamesema kuwa katika kilimo chao wanakabiliwa na changamoto kubwa ya mazao yao kunyakua pamoja na mabadiliko ya hali ya hewa.

WAKULIMA WATAKIWA KUFUATA USHAURI UNAOTOLEWA NA WATAALAM WAKULIMA WATAKIWA KUFUATA USHAURI UNAOTOLEWA NA WATAALAM Reviewed by safina radio on May 11, 2018 Rating: 5

No comments