CHANJO YA KICHAA CHA MBWA YAZINDULIWA MKOANI KILIMANJARO.


Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa FAO kwa kushirikiana na uongozi wa Mkoa wa Kilimanjaro limezindua kampeni ya chanjo ya kichaa cha mbwa na paka ambapo mbwa elfu thelathini na mbili watapatiwa chanjo hiyo.

Image result for PICHA YA MBWA

Akizungumzia kampeni hiyo katika kata ya Kindi wilaya ya Moshi Afisa Mwandamizi kutoka FAO Farus Rafina amesema kuwa wamiliki wa Mbwa pia watapewa elimu ya kukabiliana na ugonjwa huo wa kichaa cha Mbwa.

Akitoa taarifa ya ugonjwa wa kichaa cha mbwa kwa Mkoa wa Kilimanjaro Daktari wa Mifugo mkoani humo Dk. Emanuel Lema amesema kuwa kwa kipindi cha mwaka 2017/2018 mbwa wapatao 570 wamebainika kuwa na kichaa cha mbwa huku watu zaidi ya elfu nane waking’atwa na mbwa.

Akishuhudia Uzinduzi wa Chanjo hiyo Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Nghwira amesema kuwa uzuiaji na udhibiti wa mfumo wa chanjo utazuia ugonjwa huo kwa binadamu.

CHANJO YA KICHAA CHA MBWA YAZINDULIWA MKOANI KILIMANJARO. CHANJO YA KICHAA CHA MBWA YAZINDULIWA MKOANI KILIMANJARO. Reviewed by safina radio on May 04, 2018 Rating: 5

No comments