RAIS MAGUFULI ATAKA HALMASHAURI ZOTE NCHINI KUANZISHA MIFUKO YA DAWA.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dk. John Pombe Magufuli amezitaka Halmashauri zote Nchini kuanzisha mifuko ya dawa ili kurahisisha manunuzi ya dawa, Vitendea Kazi mbali mbali pamoja na vifaa vingine vya matibabu.

Image result for RAIS MAGUFULI IRINGA

Dk. Magufuli ametoa agizo hilo leo Mkoani Iringa wakati wa Hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi la Hospitali ya Wilaya ya Kilolo, ujenzi utakaogharimu kiasi cha  shilingi Bilioni 4.2 ambayo itakuwa na X-rays, pamoja na chumba cha upasuaji.

Aidha, ametoa wito kwa wananchi kujiunga na Bima ya Afya ambayo itawarahisishia  kupata huduma za Afya kwa urahisi pamoja na kupunguza gharama za upatikanaji wa matibabu,ambapo pia serikali imetenga  jumla ya shilingi bilioni 50 kwa ajili kununuliwa vifaa vya Hospitali  kote nchini.

Kwa upande wake waziri wa nchi ofisi ya rais tawala za mikoa na serikali za mitaa Mh Suleman Jaffo amesema kuwa kukamilika kwa hospitali hiyo kutaongeza idadi ya hospitali za wilaya hapa nchini kufikia 77.

Amesema kuwa kwa sasa serikali inaendelea na ujenzi wa hospitali za wilaya nne hapa nchini  ikiwemo wilaya za Buchosa,Siha na Kilolo huku ikiendelea na ujenzi wa vituo vya afya 208.

RAIS MAGUFULI ATAKA HALMASHAURI ZOTE NCHINI KUANZISHA MIFUKO YA DAWA. RAIS MAGUFULI ATAKA HALMASHAURI ZOTE NCHINI KUANZISHA MIFUKO YA DAWA. Reviewed by safina radio on May 02, 2018 Rating: 5

No comments